Type Here to Get Search Results !

Mtendaji wa Mtaa Daraja la III - (NAFASI 14) Halmashauri ya Mji Newala

Mtendaji wa Mtaa Daraja la III - (NAFASI 14) Halmashauri ya Mji Newala


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Newala anapenda kuwatangazia Watanzania wote wenye sifa kutuma maombi kwa kazi ifuatayo:-

Mtendaji wa Mtaa Daraja la III - (NAFASI 14)


Sifa za Kitaaluma kwa mwombaji

  • Awe amefaulu Kidato cha nne (IV) au sita (VI)
  • Awe amefaulu mafunzo ya Astashahada (Cheti)  "NTA Level 5" katika fani zifuatazo:- Utawala, Sheria, Elimu ya Jamii, Usimamizi wa Fedha, Maendeleo ya Jamii au Sayansi ya jamii kutoka Chuo chochote kinachotambulika Serikali.


Kazi na Majukumu ya Mtendaji wa Mtaa

  • Kuwa Katibu wa Kamati ya Mtaa
  • Mtendaji Mkuu wa Mtaa
  • Mratibu wa utekelezaji wa Sera na Sheria zilizotekelezwa na Halmashauri katika Mtaa
  • Kuwajibika kwa Mtendaji wa Kata


MSHAHARA

Cheo cha Mtendaji wa Mtaa daraja la III kina mshahara wa TGS B kwa Mwezi


MASHARTI YA JUMLA

  • Mwombaji awe Mtanzania mwenye umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 45
  • Mwombaji aambatanishe cheti cha kuzaliwa
  • Mwombaji ambaye ni mtumishi wa Umma apitishe barua yake ya maombi kwa mwajiri wake
  • Mwombaji aambatanishe maelezo yake binafsi yanayojitosheleza (CV) yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya Wadhamini (referees) watatu wa kuaminika pamoja na namba zao za simu.
  • Maombi yote yaambatanishwe na nakala za vyeti vya elimu na taaluma kutoka vyuo vinavyotambulika na Serikali
  • Testimonials, Provisional results, Statements of results n.k hazikubaliki
  • Waombaji waweke picha pamoja na passport size katika barua zao za maombi
  • Waombaji wote ambao wamesoma nje ya nchi wahakikishe vyeti vyao vinafanyiwa ulinganishi na TCU na NACTE
  • Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 03/06/2022 saa tisa alasiri

Barua zote zitumwe kwa anuani iliyopo hapa chini

MKURUGENZI WA MJI,
HALMASHAURI YA MJI NEWALA,
186 BARABARA YA MASASI,
MTAA WA TUPENDANE,
S.L.P  39,
63482 NEWALA.

Post a Comment

0 Comments