Type Here to Get Search Results !

Mtendaji wa Kijiji III - Nafasi za kazi mpya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala May, 2021

TANGAZO LA NAFASI ZAKAZI

Mtendaji wa Kijiji III - Nafasi za kazi mpya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala May, 2021


1. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Msalala kupitia kibali cha ajira mbadala chenye Kumb.Na.FA.170l376rc1f8"146 cha tarehe 06 April, 2021 kilichotolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishiwa Umma na Utawala Bora, anatangaza nafasi zakazi kwa wananchi wa Tanzaniawenye sifa na ujuzi wa kujaza nafasi zifuatazo:-

2. MTENDAJT WA KIJlJl III - NAFASI MOJA (1)

2.1 Sifa za Muombaji,

Awe na elimuya kidato cha Nne (lV) au Sita (VI) aliyehitimu mafunzo ya Astashahada/Cheti katika moja ya fani za Utawala, Sheria, Elimu ya Jamii, Maendeleo ya Jamii na Sayansi ya Sanaa kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Dodoma au chuo chochote kinachotambulika na serikali

2.2. Ngazi ya Mshahara

TGS. B, kwa kuzingatia viwango vya Serikali

2.3. Majukumu ya Kazi

l. Afisa Masuuli na Mtendaji Mkuu wa Serikali ya Kijiji

ll. Kusimamia Ulinzi na Utawala Bora kwa Raia na mali zao. Kuwa mlinzi wa amani na msirnamiziwa Utawala bora katika Kijiji.

lll. Kuratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa mipango ya maendeleo katika Kijiji

lV. Katibu wa Mikutano na Kamati zote za Halmashauri ya Kijiji

V. Kutafsiri na kusimamia Sera, Sheria na Taratibu

VI. Kuandaa taarifa za utekelezali wa kazi katika eneo lake na kuhamasisha wananchi katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya kuondoa njaa, umasikini na kuongeza uzalishaji mali.

Vll. Kiongozi wa Wakuu wa Vitengo vya Kitaalam katika Kijiji

Vlll. Kusimamia, kukusanya na kuhifadhi kumbukumbuu zote na nyaraka za Kijiji

lX. Kuwa mwenyekiti wa kikao cha wataalam waliopo katika Kijiji

X. Kupokea,kusikiliza na kutatua migogoro ya wananchi

Xl. Kusimamia utungajiwa Sheria ndogo zaKijiji na

Xll. Atawajibika kwa Mtendajiwa Kata


3. MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II - NAFAST MOJA (1)

3.1. Sifa za Muombaji,

Awe amehitimu kidato cha Nne (IV) au Sita (VI) na mwenye cheti cha utunzaji kumbukumbu katika mojawapo ya fani za Afya, Masjala, Mahakama na Ardhi.

3.2. Ngazi ya Mshahara,

TGS.B Kwa kuzingatia viwango vya serikali

3.3. Majukumu ya Kazi,

l. Kutafuta kumbukumbu/nyarakalmafaili yanayohitajika na wasomaji

Il. Kudhibiti upokeaji, uandikishaji wa kumbukumbu/nyaraka

lll. Kuchambua, kuorodhesha na kupanga kumbukumbu/nyaraka katika makundi kulingana na somo husika (Classification of boxing) kwaajili ya matumizi ya Ofisi

lV. Kuweka/kupanga kumbukumbu/nyaraka katika reki ( file racks/cabinets) katika masjala/vyumba vya kuhifadhia kumbukumbu

V. Kuweka kumbukumbu (barua,nyaraka n.k.) katika mafaili

V. Kushughulikia maombi ya kumbukumbu/ nyaraka kutoka Taasisi za Serikali.

4. MASHARTI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE

I. Waombajiwote wawe Raia wa Tanzania wanye umri usiozidi miaka 45

ll. Waombaji waambatanishe cheti cha kuzaliwa

Ill. Waombaji waambatanishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anuani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (Referebs) wa kuaminika 

IV. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo na vyeti vya kidato cha Nne na Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.

V. Testimonials, "Provision Resu/b'i "statements of Results", hati ya matokeo ya kidato cha Nne na Sita HAVITAKUBALIWA

VI. Waombaji waambatishe picha moja "Pasport Size" ya hivi karibuni

VII.  Mwisho wa kutuma maombi nitarehe 1310512021

NB; Tangazo hili linapatikana katika tovuti ya Halmashauri ded@msalaladc.go.tz, tovuti ya secretarieti ya ajira www.ajira.go.tz na katika mbao za matangazo za Halmashauri.

Maombi yote yatumwe kwa:

Mkurugenzi Mtendaji (W)

Halmashaui ya Wilaya Msalala

S.L.P 16

KAHAMA

Post a Comment

0 Comments